Kubariki ni kunena makusudio au fadhila ya Mungu kwa mtu au hali fulani.
Tunapofanya hivyo katika imani, tunachochea nguvu za Mungu kubadilisha mtu (pamoja na sisi) tukiwemo au hali, kutoka alipo sasa hadi anapotaka Mungu awe.
Kila Mkristo ana mamlaka na nguvu ya kuwabariki wengine katika jina la Bwana na kuona maisha na hali ikibadilika. Nguvu za baraka ni za mwujiza; ni uwepo na kazi ya Roho Mtakatifu, zikitoa furaha, amani, ufanisi na matokeo mazuri na kutoa afya, mafanikio na ulinzi.
Katika hiki kitabu kidogo, utapata kugundua jinsi kubariki kufanyavyo kazi na kujifunza jinsi ya kuwabariki wale ambao hukulaani au kukutusi, jinsi ya kumbariki mume au mke, watoto wako, makao yako na wewe mwenyewe, jinsi ya kubariki mahali pako pa kazi, shamba lako na jumuia yako – na hata Mungu Mwenyewe.
Unaweza kuibadilisha dunia yako.
|